Powered By Blogger

Jumamosi, 6 Septemba 2025

KILIMO CHA MAHINDI 2025

  Habari ndugu mkulima 

  Ni wakati wa kilimo sasa ni vyema kuandaa shamba mapema ili kuendana na mfumo wa hali ya hewa kwa mvua kuwahi au kuchelewa

  Napenda kuwakumbusha kujinga kwenye mfumo wa ruzuku wa segikali ili kuweza kupata mbegu na mbolea kwa bei nzuri yenye punguzo la serikali.

  Kilimo cha mahindi ni kilimo mama kwa Tanzania mana ndilo zao letu kuu la chakula. Ni vyema kuendelea kujifunza na kulifanya zao la kibiashara pia ili kujitengenezea kipato zaidi na zaidi kupitia zao hilii

Ili kufikia malengo ni lazima kuwa na mpango kazi wa uzalishaji wenye tija 

1.fahamu unataka kulima eneo gani 

2.fahamu ukubwa wa eneo unalotarajia kulima zao husika

3.anda bajeti kulingana na ukubwa wa eneo ukijumuisha shuguli zote za uzalishaji utakazofanya uwapo shamanic

4.uwe na nguvukazi ya kutosha kwa ajili ya kuhudumia mazao shamani

5.andaa mbegu nzuri 

6.andaa shamba kwa wakati kabla mvua hazijaanza kunyesha hii itasaidia kupanda kwa wakati mazao yako

7.hakikisha mbolea ya kupandia kukuzia na kubebeshea ipo tayr 

Mkulima ukishaanda haya mambo saba muhimu sasa unaweza anzisha kilimo chenye tija cha zao la mahindi 

Karibu kwa makala ya pili kuhusu namna ya kupanda zao la mahindi kwa utaalam 


Imeandaliwa na 

Robin praise kashanga

Mtaalamu wa maswala ya kilimo na ufugaji 

Kwa mawasiliano 

0617994897,

Email  robinpraise5@gmail.com 


Jumatatu, 3 Aprili 2023

Jinsi ya kuandaa kitalu cha miwa

   Habari ndugu msomaji karibu tena kwenye makala yetu ya kilimo cha miwa

Napenda leo leotuangalie ljinsi ya kuandaa kitalu kwa ajili ya kupanda miwa, yapo mambo machache ya kufwata kabula ya kuandaa kitalu cha miwa

 1/Eneo lilimwe vizuri kwa kutifuliwa kwa uhakiaka

2/chimba nyororo au mashimo nq yaingie ndwani urefu wa sentimita 30-45 kwenda chini

3/liwe eneolenye maji ya kutosha kumwagilia

4/Andaa mbolea ya kupandia  na weka kwenye .ashimo au nyororo ulizo ziandaa

5/Chukua mbegu zako ulizoziandaa vizuri kwa kuzikinga na udumvu kwa kuchemsha 

6/panda mbegu nq fukia vizuri kwa udongo wa kutoshaa

  Kitalu cha miwa kinasaidia sana kupat mbegu iliyobora na yakuweza kupanda eneo kubwaa, unapokua na kitalu utaweza kuifahamu mbegu yako kama ina shida yoyote ya ukuaji 

Kwa mawasiliano 

0686060797 

Karibu tujifunze pmoja  kujikwamua kiuchumi

Alhamisi, 5 Machi 2020



KILIMO CHAAPAI SEHEMU YA PILI

       Papai ni zao la biashara Kama tunavyo fahami pia hutumika kama lishe majumbanii kwetu
   KUHAMISHA MICHE SHAMBANI
          tunavyofahamu baada ya kuandaa Miche kwenye kitalu lazima tuihamishe shambani. Miche ya papai huhamishwa shambani pale inapokua na urefu wa sentimita 10 na kuendelea Hadi 30. Ni vyema Miche ihamishwe mapema ili kuipa uwezo mzuri wa kukua vizuri shambani.

KUANDAA MASHIMO
  lazima shimo liandaliwee vizuri pana na refu ili kuipa uwezo mzuri papai kutanuka na kiweza kujitengenezea chakula Cha kutosha. Shimo la papai linatakiwa liandaliwee kwa kimo Cha upana wa sentimita 60 na urefu sentimita 60 piaa.

UWEKAJI WA MBOLEA
  Lazima mbolea ya samadi itumike ya kutosha ili kiweza kuipa mche maisha marefu na kuhimili Hali ya udongo uliopo. Kila mche unatakiwa uwekwe plastiki moja ya mbolea ya samadi kabla ya kupanda mche, pia mwagilia maji ya kutosha kwa muda wa siku mbili ili mbolea ipoe ndo upande mche kwenye shimo lako

UMWAGILIAJI
  lazima kuwe na kiwango maalumu Cha maji kumwagilia kwenye mche unaweza kuweka kiwango kulingana na Hali ya hewa ilivyo lakin Kama hakuna joto Sana kwa siku papai inatakiwa ipate maji Lita 5 kwa siku

PALIZI
   Ni vyema kupalilia shamba lako kila wakati pale tu unapo ona magugu yameota. Ni vyema shamba Liwe Safi na pia ili mmea usipokonyane virutubisho na magugu shambani


KARIBU SANA KWA MUENDELEZO WA MAKALA HII YA KILIMO CHA PAPAI KIBIASHARA

 Asante kwa kuwa pamoja nami
  Afisa kilimo Robin praise
  Sim 0686060797
robinpraise5@gmail.com

Jumanne, 13 Agosti 2019

KILIMO CHA PAPAI

Jinsi ya kuandaa miche ya papai
  karibu tena kwenye kilimo pendwa sana tanzania cha papai ambacho kinafaida ya kutosha sana
leo tutaangalia jinsi ya kuandaa miche ya papai tu.
  Mbege za papai ni mbege ambazo zinachukua mda kidogo hadi kuchipua kwenye kitalu. hivyo zipo njia maalumu na bora za kufanya ili kuweza kuandaa mbegu zako. Nazo ni ;
-loweka mbegu zako na maji safi kwa muda wa siku tatu, huku ukibadilisha maji kila baada ya masaa 24 ai siku moja
-baada ya siku tati zitoe na uziweke kwenye kitambaa safi chenye matirio ya pamba
- funika vizuri ni uhakikishe hazipakiani kila moja iwe na nafasi yake
-kitambaa kiwe na unyevu na fukia kwa ondongo kidogo ili kuifanya iwe na joto iweze kupasuka haraka
-hakikisha kila siku jioni unamwagilia ile sehemu uliyofukia kitambaa chenye mbegu
 - andaa viriba vyako tayari kabla mbegu hazijapasuka(kuchipua)
- mbegu zitachukua siku 5-8 kuanza kuchipua na unatakiwa kuanza kuhamisha zile zilizokua tayari zote
- pulizia dawa za kuua wadudu wa kwenye udongo kabla hujahamisha mbegu kutoka kwenye kitambaa
- zoezi hili lifanyike siku 2-3 kabla ya kupanda miche kwenye viriba
-tumia kitu chenye ncha kali il usijevunja mizizi wakati wa kupanda kwe viriba
fukia kidogo sana kwa mbaliii
-mwagilia vizuri kwa upole usijechimba mbegu na maji

mfano wa miche ya papai;

1;1 hiki ni kitalu cha papai siku mbili baada ya kuhamisha mbegiu hapo


 1;2 hapo ni baada ya siku 5 baada ya kuhamisha mbegu za papai
     karibun kwa ushauri na kufanyiwa kazi za usimamizi wa shamba. Tupo Kigamboni (kibada) Dar Es Salaam
  MICHE YA PAPAI PIA INAPATIKANA KARIBUNI WOTE( TUNAFIKA KOTE TANZANIA)

imeandaliwa na
Mtaalamu wa kilimo
  Robin Praise Kashanga
kwa mawasiliano
0686060797
email; robinpraise5@gmail.com
facebook; robin praise
insagam; agribusness-tanzania or robin-praise
  KILIMO CHA MIWA SEHEMU YA 2
karibu tena katika sehemu ya pili ya kujifunza makala ya kilimo cha miwa;
 
KUPANDA
   baada ya kuandaa mbegu yako vizuri unatakiwa kuipanda kwa wakati. shamba linatakiwa liwe limeandaliwa vizuri kwa mifereji au mashimi mazuri ili uweze kuufukia vizur usiungue na jua wakati wa jua kali.

NAFASI (SPACING)
    ni vyema kuweka nafasi nzuri kati ya msitari na mstari au shina ana shina la mua ili kuupa nafasi nzuri kuendelea kuzaliana na pia kuweka nafasi nzuri wakati wa palizi uweze kupalilia vizuri bila kuijeruhi mizizi yake. Unashauriwa kuweka nafasi ya mita moja kati ya mstari na mstari wa miwa au cm 75

UMWAGILIAJI
   Miwa inahitaji maji ya kutosha ili iweze kuzaliana vizuri shamban kwako na kuweka maji na sukari ya kutosha. angalizo        pindi unapopanda muwa tu unatakiwa kumwagili kila siku kwa siku 5-7 ili kuwezesha muwa uchipue haraka na vizuri. Ziko njia mbali mbali za umwagiliaji kwa kufungua maji kwenye bwawa na kumwagilia kwa jembe au kumwagilia kwa mashine
   ni vyema kama huna mashine uweki vizuri miundombinu yako ya umwagiliaji ili kuweza kupata urahisi wakati wa kumwagilia.

MBOLEA
   ni vyema kutumia mbole zifuatazo kwa ajili ya kupandia
       1. samadi kama inapatikana kwa wingi itumike kwa kupandia
       2. DAP
       3. SA
 Kwa mbolea za kukuzia ni vyema kutumia kama
    - URE
    - CAN
    - MOP
Pia unaweza kutumia mbolea za kampuni ya YARA KULINGANA NA MAELEKEZO YA MUUZAJI NA KAMPUNI YENYEWE

PALIZI
    ni muhimu kufanya palizi mapema kwenye miwa ili kufanya uzalishaji wa miwa kuwa vizuri na kuzaa kwa wingi pia hupunguza magonjwa kwenye miwa.
unaweza fanya palizi kwa nyia 2
1. kupalilia kwa jembe la mkono
2. kutumia madawa
   Baadhi ya dawa za magugu ni
- Diuron
- Volismer
-Grayphasety (round up)
   kwa matumizi nya dawa hizi tafadhali usitumie bila kupata maelekezo kutoka kwa mtaalamu wa kilimo.

KUKOMA NA KUVUNA
   Miwa huchukua miezi 10 had 13 kukomaa na kuvunwa ni vyema miwa ivunwe mapema kaabla ya kuchanua hivyo kuweza kupata sukari ya kutosha.
   miwa huchomwa kwanza ndio ivunwe ili kupandisha sukari na kupunguza takataka pindi unapopita kwenye mashine wakati wa kutengeneza sukari.

kwa maelezo zaidi karibu  kwa mawasiliano
  0686060797
email; robinpraise5@gmail.com
Robin Praise Kashanga
Dar es salaamu -Kigamboni (kibada)

Jumamosi, 11 Mei 2019

MWONGOZO JINSI YA KULIMA MIWA

KIKIMO CHA MIWA







  Miwa ni zao pendwa sana na binadamu wengi sana nchini tanzania, Miwa ni zao linalolimwa kwa ajili ya biashara na matumizi mengine kama tunda.
   nchini tanzania kilimo cha miwa hulimwa kwa baadhi ya mikoa kwa ajili ya biasahara, mikoa inayolima mua ni kama;


  - kilimanjaro
  - kagera
  - morogoro
  - pwani
 sehemu zote hizii hulima miwa kwa ajili ya kuzalisha Sukari kama bidhaa na juic kwa wakulima wadogowadogo. miwa ni zao linalochukua muda mrefu kukomaa na kuvunwa kwa ajili ya kuuzwa kiwandani ili kutengeneza sukari. Kwa wakulima wadogo wanaweza kulima miwa kwa sababu ni zao lisilo na garama kubwa kwa uendeshaji na lina faida nzuri linapostawi vizuri na mavuno kuwa mengi ya kutosha.

  Miwa hulimwa sehemu zenye maji ya kutosha mvua za kutosha ili kupunguza garama za umwagiliaji, ukumbuke kuwa miwa huhitaji maji ya kutosha ili lkuweza kuzalisha tani za kutopsha pind unapovuna. ni vyema kufwata ushauri na utaalamu kwenye kilimo hiki ili kuweza kuzalisha kiasi kikubwa cha miwa na kupata sukari ya kutosha.

  KUANDAA SHAMBA
Shamba la kupanda miwa ni vyema liandaliwe mapema na kama ni jipya kabisa inatakiwa kusafishwa kabisa na kutlew visiki vyote ndipo uanze kulima, unatakiwa kulima mara mbili ndipo upitishe jembe la kusawazisha ili shamba liukae vizuri. Ikumbukwe kwamba kilimo cha mua kinataka aridhi iliyo laini na tifutifu ili kuupa urahisi mua kupeleka mizizi mbali kujitafutia chakula na kukua kwa urahisi.

   KUANDAA MBEGU
 Mbegu ya miwa inatakiwa kuandaliwa mapema sana kwa kumwagiliwa sana ili iwe laini vizuri na iweze kuchipua haraka pindi inapopandwa. Ni vyema mbegu ivunwe kwa wakati wa kupanda ili isije nyauka na kuykauka kabla ya kupanda. Mbegu ya uma inatakiwa kukatwa katika pingili ndogo ndogo tatu hadi nne kuiweka tayar kwa kupandwa

kwa leo tutaishia hapo tutaendelea kwa wakat mwingine na makala yetu ya kilimo cha miwa. TUNASHIDWA KUTUMA MAKALA MARAKWA MARA KULINGANA NA MAZINGIRA YA MASHAMBANI HUWA MTANDAO WA INTERNET UNASUMBUA KIDOGO ILA NATUJITAHDI WAPENDWA WANGU
    kwa ushauri na msaada wa mazao mengine wasiliana nai kwa
no0686060797

email;robinpraise5@gmail.com

Jumanne, 2 Oktoba 2018

UFUGAJI WA KUKU

   JINSI YA KUTUNZA VIFARANGA WIKI 1-5
           Kuku ni ndege wafugwao na binadamu wengi kwa ajili ya matumizi mbalaimbali ya binadamu. Mara nyingi hutumika kwa ajili ya kitoweo na kwa biashara pia. wafugaji wengi hupenda kufuga kuku maana ni mwepesi kumtunza na hana garama kubwa za utunzaji ukilinganisha na wanyama wengine wafugwao. leo tutaangali jinsi ya kuwalea vifaranga had wafae kuwa kuku wakubwa;
Nyumba ya vifaranga;
      nyumba ya vifaranga inatakiwa kuwa karibu na nyumba ya kuishi ili uweze kuwaangalia vifaranga kwa ukaribu zaidi, ijengwe kwenye sehemu iliyotulia kulingana na mwelekeo wa upepo na kuta zisiingize baridi sana pia iwe na eneo la kutosha kulelea vifaranga.
  mfano wa nyumba ya vifaranga iliyotengenezwa na mfugaji mwenyewe

             nyumba hiyo imejegwa maalumu kwa ajilinya kutunzia vifaranga katika ustadi mzuri kabisa.
Baadhi ya wafugaji hutengeneza nyumba za kufugi ilimradi katengeneza bila kutumia vipimo au ufanisi mzuri ili kulea vifanganga vizuri.
   mfano wa nyumba ya vifaranga ambayo haijatumia ufanisi wowote kulingana na taratibu na kanuni za kulea na kutunza vifarnga ;
vifaranga hutoka wakati wote na kuzurura hivyo ni hatari kwa wanyama wakali kama vicheche mwewe na wengine wanaoweza kuwadhuru vifaranga . ni vyema kutengeneza banda bora kwa ajili ya kufugia vifaranga kwa uangalifu mzuri kukwepa hasara.

  Vyombo kwenye nyumba ya vifaranga; 
       ni muhimu kuweka vifaa safi kwenye nyumba ya vifaranga kwa ajili ya kuwalishia na kuwalelea. kipo kitu kinaitwa kitalu hiki ni kwa ajili ya kutunzia vifaranga visitawanyike ndani ya banda. taa ya chemli, jiko la mkaa pia ni vifaa muhimu vya kulelea vifaranga pindi wawapo wadogo banadani bila kuwa na mama yao.
chanjo na tiba
    vifaranga vinatakiwa kupewa chanjo kulingana na ratiba ya chanjo inavyotaka pindi tu wanapoanguliwa toka kwenye yai lake. wafugaji wengi hawapend kufuata utaratibu wa chanjo ndo maana wengi huambulia hasara pale magonjwa ya milipuko yanapotokea . ni vyema kumtumia mtaalamu kwa ajili ya maelekezo jinsi na kupata na kutumia chanjo kwa usahihi ili kukwepa kuingia hasara kwa matumizi mabaya ya dawa.
   unapo ona tofauti kwenye kuku wako unashauriwa kutumia dawa mapema na kuwatenga fifaranga wote wenye dalili ya kuumwa ili kukwepa kuwaambukiza vifaranga wengine ndani ya banda lakoooo kama mfugaji.


Imeandaliwa na
ROBIN PRAISE KASHANGA
Simu; 0768092549, 0715876743
email; robinpraise5@gmail.com

  kwa mfugaji anaetaka mwongozo wa ufugaji wa wanyama wote na kilimo  tafadhali wasiliana nami na kwa namba hizo hapo juu. pia ushauri tunatoa kwa wakulima wetu wote.


TULIME KWA BIDII KUIFIKIA TANZANIA YA VIWANDA