Powered By Blogger

Jumamosi, 6 Septemba 2025

KILIMO CHA MAHINDI 2025

  Habari ndugu mkulima 

  Ni wakati wa kilimo sasa ni vyema kuandaa shamba mapema ili kuendana na mfumo wa hali ya hewa kwa mvua kuwahi au kuchelewa

  Napenda kuwakumbusha kujinga kwenye mfumo wa ruzuku wa segikali ili kuweza kupata mbegu na mbolea kwa bei nzuri yenye punguzo la serikali.

  Kilimo cha mahindi ni kilimo mama kwa Tanzania mana ndilo zao letu kuu la chakula. Ni vyema kuendelea kujifunza na kulifanya zao la kibiashara pia ili kujitengenezea kipato zaidi na zaidi kupitia zao hilii

Ili kufikia malengo ni lazima kuwa na mpango kazi wa uzalishaji wenye tija 

1.fahamu unataka kulima eneo gani 

2.fahamu ukubwa wa eneo unalotarajia kulima zao husika

3.anda bajeti kulingana na ukubwa wa eneo ukijumuisha shuguli zote za uzalishaji utakazofanya uwapo shamanic

4.uwe na nguvukazi ya kutosha kwa ajili ya kuhudumia mazao shamani

5.andaa mbegu nzuri 

6.andaa shamba kwa wakati kabla mvua hazijaanza kunyesha hii itasaidia kupanda kwa wakati mazao yako

7.hakikisha mbolea ya kupandia kukuzia na kubebeshea ipo tayr 

Mkulima ukishaanda haya mambo saba muhimu sasa unaweza anzisha kilimo chenye tija cha zao la mahindi 

Karibu kwa makala ya pili kuhusu namna ya kupanda zao la mahindi kwa utaalam 


Imeandaliwa na 

Robin praise kashanga

Mtaalamu wa maswala ya kilimo na ufugaji 

Kwa mawasiliano 

0617994897,

Email  robinpraise5@gmail.com 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni